WELCOME HMC

2 / 3
3 / 3
3 / 3
2 / 3
Caption Two
3 / 3
Caption Three

Tuesday 11 April 2017

LIST YA MARAIS TAJIRI BARANI AFRIKA

9. Robert Mugambe
rais wa Zimbabwe amekuwa madarakani kwa takribani miaka 25 richa ya chaguzi znazofanyika nnchini humo lakini hadi hii leo bado anashikilia madaraka, anautajiri wa dola million kumi 10 za kimarekani.

8. General Idrid Deby Itno
huyu ni mwanasiasa kutoka Chad ambae amekuwa madarakani toka mwaka 1990, mwezi October mwaka 2006 jarida la Forbes lilitaja Chad kuwa ndio nnchi inayoongoza kwa rushwa duniani.ruzuku Kutoka kwenye mradi wa mafuta wa Chad-Cameroon na bomba la mafuta ambapo fedha zake zilikusudiwa kupambana na njaa pamoja na kukuza miradi ya maendeleo badala yake alitumia fedha hizo kununua majeshi na kukuza nguvu ya Idris ambae anakadiliwa kuwa na utajiri wa dola milioni hamsini 50 za kimarekani.

7. Goodluck Ebele Jonathan
huyu ni rais wa Nigeria anautajiri wa dola milioni 100 mia moja  za kimarekani.


6. King Mswati III
Huyu ni mflame kutoka Swaziland anayesifika kwa kuwa na wake wengi akiwa anamiliki utajiri wa Dollar za kimarekani $100 MILLION

5. Poul Biya
huyu ni mwanasiasa kutoka Cameroon ambae amekuwa akiingoza nchi hiyo toka November 6 mwaka 1982 rekodi inayomfanya kuwa miongoni mwa marais walioongoza kwa muda mrefu duniani kwa kipindi cha miaka 31, anamiliki kiasi cha dola milioni 200 za kimarekani inasemekana Poul Biya ndiye tajiri mkubwa huko Cameroon lakini pia imeripotiwa kuwa msafara wake ndio msafara wa gharama kuliko kiongozi yeyote duniani hata rais wa marekani kwa kutumia sio chini ya dola elfu 40 za kimarekani

4. Uhuru Kenyatta
Uhuru Muigai Kenyata huyu ni rais wa Kenya alizaliwa octoba 26 mwaka 1961 akiwa kama rais wanne wa Kenya na wasasa.

Ameanza rasmi kazi hiyo ya urais april 9 2013, pia ni moja katio ya vijana matajiri huko Kenya anakadiliwa kuwa na dola za kimarekani milioni 500, utajili huu umetokana na kumiliki zaidi ya heka 500000 kwenye ardhi ya Kenya lakini pia akiwa mwanahisa wa makampuni ya habari, hoteli pamoja na benki.


3. Teodoro Obiang Nguema mbasongo
huyu amekuwa akiiongoza equatoliar Guinea kwa miaka 34 baada ya kumuangusha mjomba wake 1979 kwa mapinduzi ya kijeshi, inasemekana chini ya uongozi wake kwenye taifa hilo lenye utajiri wa mafuta wananchi hawanufaiki kabisa na utajili huo na kuishi chini ya dola moja kwa siku, mototo wake wa kiume anafuata nyayo zake kwa kuishi kwenye bangaloo lenye thamani ya dola milioni 34 za kimarekani huko Malibu na gari aina ya Bugatti veyrons yenye thamani ya dola milioni 1.7 za kimarekani.

2. Mohamed wa VI wa Morocco
huyu aliwahi kuwa mfalme wa Morocco miaka 15 iliyopita kutoka kwenye familia ya ktajili aliweka ahadi za kuongeza ajira na kupunguza umaskini pamoja na rushwa na baadae kufanikiwa hii ilimfanya apendwe saana kuwa kiongozi mkweli kwa raia wake anautajiri wa dola billion 2.5 za kimarekani.

1. Jose Eduardo Dos Santos
amekuwa madarakani kwa takribani miaka 34 kama rais wa Angola anautajili wa dola bilioni 20 za kimarekani kama utajili binafsi, huku mwanae Isabel Dos Santos akitajwa kuwa mwanamke tajiri Afrika na dunia kama mwanamke mweusi tajiri kwa kumiliki zaidi ya dola bilioni 3.4 za kimarekani kama utajiri binafsi

No comments:

Post a Comment