WELCOME HMC

2 / 3
3 / 3
3 / 3
2 / 3
Caption Two
3 / 3
Caption Three

Tuesday 16 February 2016

SEMINA YA SELF AWARENESS YAKUTANISHA VIJANA MBALIMBALI KATIKA CHUO CHA HABARI MAALUM

  Vijana kutoka vyuo mbalimbali Jijini Arusha wamekutana katika Semina ilikuwa na ujumbe wa Self awereness is more than money iliyotelewa na Mjasiriamali Bi Gracy Lyimo Pamoja na Ndugu Maxwell Chaila ambaye alifundisha kuhusu   Self Employment  can take your life into first class,Semina hiyo ilifanyika katika viunga vya Chuo cha Habari Maalum Jijini Arusha Mapema wiki iliyopita.

Na Diu Mwiko

Bi Gracy Lyimo akielezea kuhusu jinsi gani mtu anaweza akajitambua  mwenyewe..(Picha Na Nickson Mafuru)

Aidha katika Semina hiyo Bi Gracy amewataka vijana hao kujitambua pamoja na kutambua malengo yao na kuyafanyia kazi.

Nae msemaji wa pili katika semina hiyo Ndugu Maxwell Chaila aliongelea suala la kujiajiri mwenyewe na kusema kuwa linaweza kukuweka katika daraja la juu(Self employment can take your life into first class).

Katika semina hiyo Ndugu Maxwell amewataka vijana kufikiria kujiajiri na sio kutegemea kuajiriwa hali ambayo itawafanya kuwa huru.

Ndugu Maxwell Chaila mmiliki wa kampuni ya Ulinzi Jijini Arusha akifafanu kuhusu mambo matatu ambayo ni muhimu ili mtu aweze kujiajiri mwenyewe ambayo ni kujenga nidhamu,malengo pamoja na kujiunga na wajasiriamali.(Picha na Nickson Mafuru)















Akiwakaribisha wasemaji hao mkuu wa Chuo cha Habari Maalum Bwana Jackson Kaluzi amesema kuwa semina kama hizo ni jambo la msingi sana kwani linaenda sambamba na maono ya Chuo hicho kitu ambacho kitakuwa msaada mkubwa kwa wanafunzi pindi watakapo hitimu masomo yao.

Mkuu wa Chuo cha Habari Maalum Bwana Jackson Kaluzi wa kwanza kulia akifuatilia kwa makini Semina hiyo,wa pili kutoka kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma Ndugu Lazorus Laiser,na wa tatu ni Ndugu Nestory Ihano Mkuu wa kitengo cha Uongozi na Utawala na pia ni mlezi wa wanafunzi chuoni hapo.(Picha na Nickson Mafuru).














Mwalimu Jastine Peter kutoka chuo  cha Habari Maalum aliyefanikisha kufanyika kwa semina hiyo akishirikiana na serikali ya Wanafunzi kutoka Chuo cha Habari Maalum pamoja na Chuo Kikuu Cha Mount Meru akitoa shukrani kwa wageni .(Picha Na Nickson Mafuru)
Burudani pia hazikukosekana ,mmoja wa wanafunzi kutoka katika chuo cha Habari Maalum anaekwenda kwa jina la Depper akionesha kipaji chake cha kuimba wakati wa semina hiyo(Picha Na Nickson Mafuru)


Baadhi ya Washiriki wa Semina hiyo wakiwa katika picha ya Pamoja mara baada ya semina hiyo.(Picha na Nickson Mafuru)

1 comment: