WELCOME HMC

2 / 3
3 / 3
3 / 3
2 / 3
Caption Two
3 / 3
Caption Three

Sunday 16 April 2017

Kama Unabomoa Misingi Hi, Hutaweza Kufanikiwa Tena

Tumia kile ulichonacho kwa uhakika na vizuri kabisa. Acha kujidanganya kwamba unataka mafanikio makubwa wakati hata ile misingi ya kutengeneza mafanikio makubwa unaiharibu hovyo hovyo.

Haiwezekani eti unasema unataka mafanikio makubwa wakati unatumia muda, pesa na nguvu zako hovyo, ambapo vitu hivyo kwa pamoja vingekusaidia kufikia mafanikio makubwa kama ungevitumia vizuri na kwa busara.

Hata Pesa unazozipata hazijiamulii zenyewe kwamba ‘sasa mimi pesa ninakwenda kununua kitu hiki au kile.’ Wewe ndiye mwenye jukumu la kupanga pesa zako zitumike wapi na kwa sababu ipi.
Soma; Tabia Tatu (3)  Muhimu Unazotakiwa Kuziendeleza, Ili Kufanikiwa.

Sasa kama hiyo iko hivyo, kwa nini unafanya maamuzi mabovu ambayo yanakupotezea pesa nyingi na kwa kiasi kikubwa? Kuwa makini sana na matendo yako ili yasikupotezee pesa ambayo ni moja rasilimali muhimu kukusaidia kufanikiwa.

Hapo ulipo najua una pesa za kiasi fulani hata kama ni ndogo, najua una muda na nguvu fulani, sasa kwa nini hivi vitu usivitumie kwa uangalifu ili viweze kukusaidia kukupa mafanikio makubwa na badala ya kuvipoteza tu kiholela.

Watu matajiri, wanajua namna ya kutunza pesa zao vizuri, kwa nini wewe usiwe miongoni mwao? Huna pesa za kutosha si kwa sababu pesa zinakukimbia bali ni kutokana na matendo yako yanayofukuza pesa.

Kitu cha kufanya jiulize, ni hatua zipi utaweza kuzichukua ili kuweza kulinda hata zile rasilimali zako za kukusaidia kufanikiwa ambazo ni pesa, muda na nguvu zako. Kama hujui tafuta watu wenye mafanikio kisha wafatilie na ujue nini cha kufanya.

Lakini kitu ambacho nataka uelewe hapa jifunze sana kutumia kile kidogo ulichonacho kikusaidie kufanikiwa. Najua unaelewa wapo watu ambao wanadharau sana hasa ikiwa wanacho kile kidogo.
Watu hawa mara nyingi hawajui thamani ya kutumia kile kidogo walichonacho. Iwe ni pesa kidogo watazitumia hovyo mpaka zitakwisha. Iwe ni muda kidogo pia watautumia hovyo hata bila kupata faida ya muda huo.

Kwa kuwa wewe umeshalijua hili leo, amua kutumia kiasi kidogo cha pesa ulichonacho kwa busara ili kikusaidie kutengeneza pesa nyingi. Pia amua kutumia muda, nguvu zako au chochote ulichonacho ambacho unaona ni kidogo kikusaidie kufanikiwa.

Hata Musa wakati anawaongoza wana wa Israeli kuvuka bahari ya shamu, alitumia fimbo aliyonayo kupiga bahari na ikagawanyika, hapo ndipo wana wa Israeli wakaokolewa.

Leo hii ni kipi ambacho huna. Najua una kidogo ulichonacho ila hujaona sana kama kinaweza kukusaidia. Sasa hebu anza leo kukiangalia kwa jicho la tofauti ili kikusaidie kujenga mafanikio makubwa.

Kabla sijaweka kalamu yangu chini pengine nikwambie hivi, kama unabomoa misingi hii ya kushindwa kutumia kile angalau kidogo ulichonacho kwa busara na vizuri…kufanikiwa kwako itabaki kuwa hadithi.

Hiyo iko hivyo kwa sababu, mafanikio yanajengwa na vitu vidogo vidogo sana ambavyo mwanzo huonekana si kitu wala si chochote, lakini vitu hivyo ndivyo hatimaye vinavyofanya mafanikio yakaonekana kwa nje.

Sasa wewe ni nani hadi ufanikiwe wakati unajiona kabisa unavunja sheria za asili za mafanikio? Huwezi kufanikiwa. Ila kikubwa utakachofanya ni kujidanganya tu kwamba ipo siku lazima nitafanikiwa.

Mpaka hapo ulipo jiulize je, hicho ulichonacho unakitumia kwa vizuri ili kikusaidie kupata kingine kikubwa? Lakini ikiwa unataka kufika katika ngazi fulani ya mafanikio, huku hapo ulipo hujiwekei misingi imara hutaweza kufika huko.

Kila wakati jitathimi katika kila eneo unalotaka kufika kwa kujiuliza je, kile kidogo ulichonacho unakitumia ili kukusaidie kufanikiwa? Ukiweza kupangilia vizuri matumizi ya kidogo ulichonacho na kuhakikishia UTAFANIKIWA

No comments:

Post a Comment