WELCOME HMC

2 / 3
3 / 3
3 / 3
2 / 3
Caption Two
3 / 3
Caption Three

Thursday 13 April 2017

Trump abadili msimamo kuhusu NATO

Trump amesema kuwa shirika hilo sasa lina umuhimu baada ya kuanza kukabiliana na ugaidi

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa shirika la kujihami la NATO sasa linafaa na kwamba halijapitwa na wakati hatua ambayo imewashangaza washirika wake.

Akizungumza na katibu mkuu wa shirika hilo Jens Stoltenberg katika Ikulu ya Whitehouse ,Trump amesema kuwa tishio la ugaidi limesistiza umuhimu wa muungano huo.

Ametoa wito kwa NATO kusaidia washirika wake nchini Iraq na Afghanistan.

Bwana Trump mara kwa mara amekuwa akitilia shaka umuhimu wa shirika hilo huku akilalamika kwamba Marekani inatoa kitita kikubwa cha ufadhili wake ikilinganishwa na mataifa mengine.

Sio mara ya kwanza kwa bwana Trump kulalamika kuhusu shirika hilo siku ya Jumatano.

Katika mahojiano na jarida la Wall Street alisema kuwa hataitaja China kuwa imekuwa ikishawishi sarafu yake ili kuangazia maslahi yake ,licha ya kuahidi kusema hivyo siku moja tu baada ya kuchukuwa mamlaka.

Katika mahojiano ya pamoja ya vyombo vya habari na Stoltenberg Bwana Trump alisema: katibu mkuu wa Nato na mimi tumefanya mazungumzo ya kufana kuhusu ni nini zaidi NATO inaweza kufanya katika vita dhidi ya ugaidi.

Nililalamika kuhusu hilo hapo awali na wakafanya mabadiliko na sasa wanakabiliana na ugaidi.
Nilisema NATO 'imepitwa na wakati' lakini sasa 'haijapitwa na wakati'.

Bwana Trump alisisitiza wito wake kwa wanachama wa NATO kuchanga fedha zaidi kwa shirika hilo.

No comments:

Post a Comment