WELCOME HMC

2 / 3
3 / 3
3 / 3
2 / 3
Caption Two
3 / 3
Caption Three

Wednesday 17 February 2016

Jela ya wenye misimamo mikali kujengwa Kenya












Rais Uhuru Kenyatta akizungumzia suala la ujenzi wa mahakama ya wenye misimamo mikali

Na Renalda Mwarabu

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema njia pekee ya kupunguza kuenea athari mbaya za ugaidi na madudu yake ni kupitia kuundwa jela ya aina yake itakayotumiwa kuwafungia watu wenye misimamo mikali.

Rais Kenyatta amesema kuchanganyika wafungwa wa kawaida na wale wenye misimamo mikali na magaidi kumechangia tatizo hilo kuenea na watu wengi kujiunga na makundi ya aina hiyo.
 
"Tutaunda jela maalumu kwa ajili ya watu wenye misimamo mikali. Hatutokubali fikra za ugaidi na misimamo mikali kuenezwa kupitia jela za nchi hii" amesema kiongozi huyo.
 
Ingawa hakutaja kundi lolote moja kwa moja, wachambuzi wanasema kundi la kigaidi la al Shabaab ndilo lililolengwa kwenye kauli hiyo ya Rais wa Kenya.
 
Kundi hilo limekuwa likifanya mashambulizi ya kushtukiza dhidi ya raia na maafisa wa usalama wa Kenya ndani na nje ya nchi hiyo.
 
 Shambulizi la hivi karibuni la kundi hilo dhidi ya Kenya ni lile lililotokea katika kambi ya el-Adde ambako wanajeshi zaidi ya 50 kutoka Kenya waliuawa.
 

Ikumbukwe kuwa tangu mwaka wa 2011 kundi la alshababu limekuwa likifanya mashambulizi yake nchini Kenya na kuleta maafa makubwa. (kutoka mtandaoni)

No comments:

Post a Comment