Renalda na Jane Mafupa
Friday, 4 March 2016
Museveni asema hatogawana madaraka na wapinzani
Na Renalda Mwarabu
Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema hawezi kugawana madaraka na
kambi ya upinzani kwani alishinda kihalali kwenye uchaguzi mkuu wa
Februari 18.
Akizungumza na kiongozi wa chama cha upinzani cha Farmers Party of Uganda (FPU), Meja Jenerali Benon Biraaro, Rais Museveni amesema anakaribisha pendekezo la kufanya mazungumzo na wapinzani kwa ajili ya kujadili mustakabali wa kisiasa wa taifa lakini hawezi kuunda serikali ya umoja wa kitaifa itakayowashirikisha wanasiasa wa upinzani.
Amesema uchaguzi ulikuwa fursa nzuri kwa wanasiasa kujitafutia vyeo na kama wapinzani walishindwa kuwashawishi wapiga kura, wanapaswa kusubiri hadi uchaguzi ujao na wala si kutumia njia za mkato kuingia serikalini.
Huku hayo yakijiri kuna tetesi kwamba kiongozi wa upinznai, Kizza Besigye ametoweka na hajulikani aliko. Duru za habari zinasema Besigye ambaye alikuwa chini ya kifungo cha nyumbani hayuko tena nyumbani kwake. Polisi ya Uganda imekataa kuthibitisha au kukanusha suala hilo.( Chanzo Radio Terhan)
Serikali yavipongeza Vyombo vya Habari kwa kuhabarisha jamii vyema
Na Renalda Mwarabu
Naibu
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James
Wambura amevipongeza Vyombo vya Habari kwa kuwahabarisha watanzania
vyema katika mchakato wote wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na katika
kipindi cha siku mia za kwanza za awamu ya tano ya utawala wa Mheshimiwa
Dr. John Joseph Pombe Magufuli.
Naibu
Waziri uyo ameyasema hayo alipokuwa akiongea na wadau wa Habari katika
tafrija fupi iliyoandaliwa na kampuni ya Mwananchi Communications
Limited.
“Hakika mmeonesha uwezo mkubwa, weledi na ukomavu mkubwa wa kisiasa na uzalendo kwa nchi yetu”.Alisema Bi.Wambura.
Mhe.Wambura
pia alieleza kuwa Serikali ya awamu ya tano ina dhamira ya dhati kabisa
ya kushirikiana na wadau wote vikiwemo Vyombo vya Habari, ambapo pia
mchakato wa Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ambao ulishasomwa kwa
mara ya kwanza bungeni bado Serikali inaendelea kupokea maoni ya wadau
mbalimbali juu ya namna bora ya kuboresha Muswada huo.
Naibu
Waziri uyo alikazia umuhimu wa upashaji habari na kusema ni jambo
muhimu sana katika nchi yetu na kwaiyo Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa
na Michezo iko tayari kufanya kazi na wadau wote.
“Kama
Serikali hatuwezi kuwakwepa wadau na ndio maana hata utaratibu wetu wa
kushughulikia makosa kwenye Vyombo vya Habari umebadilika. Tumekuwa ni
walezi zaidi badala ya kuwa viranja. Tunashauriana zaidi kuliko kutoa
adhabu. Tunaelimisha zaidi kuliko kusubiliana”
Naibu
Waziri uyo pia ameupongeza uongozi mpya wa jukwaa la wahariri na
kuhaidi kuwapa ushirikiano wa karibu katika kutatua masuala mbalimbali
ya Habari.
Kwa
upande wake Mwenyekiti Mtendaji wa Bodi ya Magazeti ya Mwananchi
Bw.Francis Nanai ameipongeza serikali kwa kuweka jitihada zaidi katika
kuboresha mahusiano mazuri na vyombo vya Habari na pia kwa afrika
mashariki Tanzania iko katika nafasi nzuri ukilinganisha na wenzetu
katika suala la uhuru wa vyombo vya habari.
(Chanzo Mo bog)
Ban na wasiwasi na kuenea misimamo mikali Afrika
Na Renalda Mwarabu
![]() |
Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Bwana Ban Ki Moon akitoa wasiwasi wake juu kuhusu mashambulizi ya kigaidi barani Afrika |
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ameelezea wasiwasi wake kuhusu
mashambulizi ya makundi ya kigaidi huko Burkina Faso, magharibi mwa
Afrika na kuitaka dunia isimame kukabiliana na hatari ya kuenea misimamo
mikali barani Afrika.
Ban Ki moon amesema hayo huko Ouagadougou, mji mkuu wa Burkina Faso
na kuongeza kuwa, nchi za ukanda huo zinapaswa kushrikiana kukabiliana
na matatizo mbalimbali kama vile umaskini, ukosefu wa kazi, ubaguzi na
kinga ya kutoshitakiwa baadhi ya watu.
Ban alianza ziara yake ya kuzitembelea nchi kadhaa za Afrika siku ya
Jumatano kwa kuanzia nchini Burkina Faso ambako alilakiwa na Alpha
Barry, Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo.
Jana Alkhamisi alionana na Rais Roch Marc Christian Kaboré wa nchi
hiyo, kama ambavyo alitembelea pia kituo kimoja na kuwasaidia chakula
watoto wadogo na kituo kimoja cha watoto wenye maradhi ya Ukimwi.
Mbali na Burkina Faso, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amepangiwa kutembelea pia nchi za Mauritania na Algeria.
Ziara ya Ban Ki moon inafanyika katika hali ambayo hivi karibuni
kulitokea mashambulio ya kigaidi katika mji mkuu wa Burkina Faso,
Ouagadougou na kupelekea kuuawa zaidi ya watu 30. Chanzo Radio Terhan
Subscribe to:
Posts (Atom)
Popular Posts
|
|